Mithali 6:1-5
1
Mwanangu, kama umekuwa mdhamini wa jirani yako, ikiwa umeshika mikono kwa kuweka ahadi kwa ajili ya mwingine,
2
kama umetegwa na ulichosema, umenaswa kwa maneno ya kinywa chako,
3
basi fanya hivi mwanangu, ili ujiweke huru, kwa kuwa umeanguka mikononi mwa jirani yako: Nenda ukajinyenyekeshe kwake; msihi jirani yako!
4
Usiruhusu usingizi machoni pako, usiruhusu kope zako zisinzie.
5
Jiweke huru, kama swala mkononi mwa mwindaji, kama ndege kutoka kwenye mtego wa mwindaji.
Settings