Mithali 6:6-11
6
Ewe mvivu, mwendee mchwa; zitafakari njia zake ukapate hekima!
7
Kwa maana yeye hana msimamizi, wala mwangalizi, au mtawala,
8
lakini hujiwekea akiba wakati wa kiangazi na hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9
Ewe mvivu, utalala hata lini? Utaamka lini kutoka usingizi wako?
10
Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo, bado kukunja mikono kidogo upate kupumzika:
11
hivyo umaskini utakuja juu yako kama mnyangʼanyi, na kupungukiwa kutakujia kama mtu mwenye silaha.
Settings