Skip to content
Mithali 5:18-23

Mithali 5:18-23

18
Chemchemi yako na ibarikiwe na umfurahie mke wa ujana wako.
19
Kulungu jike apendaye, kulungu mzuri: matiti yake na yakutosheleze siku zote, nawe utekwe daima na upendo wake.
20
Kwa nini mwanangu, utekwe na mwanamke kahaba? Kwa nini ukumbatie kifua cha mke wa mwanaume mwingine?
21
Kwa maana njia za mtu ni wazi kabisa mbele za Bwana, naye huyapima mapito yake yote.
22
Matendo mabaya ya mtu mwovu humnasa yeye mwenyewe; kamba za dhambi yake humkamata kwa nguvu.
23
Atakufa kwa kukosa nidhamu, akipotoshwa kwa upumbavu wake mwenyewe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options