Mithali 19:4-9
4
Mali huleta marafiki wengi, bali rafiki wa mtu maskini humwacha.
5
Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo hataachwa huru.
6
Wengi hujipendekeza kwa mtawala na kila mmoja ni rafiki wa mtu atoaye zawadi.
7
Mtu maskini huepukwa na ndugu zake wote: Je, marafiki zake watamkwepa kiasi gani! Ingawa huwafuata kwa kuwasihi, hawapatikani popote.
8
Yeye apataye hekima huipenda nafsi yake mwenyewe, yeye ahifadhiye ufahamu hustawi.
9
Shahidi wa uongo hataacha kuadhibiwa, naye amwagaye uongo ataangamia.
Settings