Skip to content
Mithali 19:10-15

Mithali 19:10-15

10
Haistahili mpumbavu kuishi katika anasa, itakuwa vibaya kiasi gani kwa mtumwa kuwatawala wakuu.
11
Hekima ya mtu humpa uvumilivu, ni kwa utukufu wake kusamehe makosa.
12
Ghadhabu ya mfalme ni kama mngurumo wa simba, bali wema wake ni kama umande juu ya nyasi.
13
Mwana mpumbavu ni maangamizi ya babaye, naye mke mgomvi ni kama kutonatona kusikoisha.
14
Nyumba na mali hurithiwa kutoka kwa wazazi, bali mke mwenye busara hutoka kwa Bwana.
15
Uvivu huleta usingizi mzito, naye mtu mzembe huona njaa.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options