Mithali 15:8-12
8
Bwana huchukia sana dhabihu za waovu, bali maombi ya wanyofu humfurahisha Mungu.
9
Bwana huchukia sana njia ya waovu, bali huwapenda wale wafuatao haki.
10
Adhabu kali humngoja yeye aachaye njia; yeye achukiaye maonyo atakufa.
11
Mauti na Uharibifu viko wazi mbele za Bwana: je, si zaidi sana mioyo ya wanadamu!
12
Mwenye mzaha huchukia maonyo; hatataka shauri kwa mwenye hekima.
Settings