Skip to content
Mithali 15:1-7

Mithali 15:1-7

1
Jawabu la upole hugeuza ghadhabu, bali neno liumizalo huchochea hasira.
2
Ulimi wa mwenye hekima husifu maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hufoka upumbavu.
3
Macho ya Bwana yako kila mahali, yakiwaangalia waovu na wema.
4
Ulimi uletao uponyaji ni mti wa uzima, bali ulimi udanganyao huponda roho.
5
Mpumbavu hubeza maonyo ya baba yake, bali yeyote akubaliye maonyo huonyesha busara.
6
Nyumba ya mwenye haki ina hazina kubwa, bali mapato ya waovu huwaletea taabu.
7
Midomo ya mwenye hekima hueneza maarifa, bali sivyo ilivyo mioyo ya wapumbavu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options