Mithali 14:28-35
28
Wingi wa watu ni utukufu wa mfalme, bali pasipo watu mkuu huangamia.
29
Mtu mwenye subira ana ufahamu mwingi, bali anayekasirika haraka huonyesha upumbavu.
30
Moyo wenye amani huupa mwili uzima, bali wivu huozesha mifupa.
31
Yeye amwoneaye maskini huonyesha dharau kwa Muumba wao, bali yeyote anayemhurumia mhitaji humheshimu Mungu.
32
Waovu huangamizwa kwa matendo yao maovu, bali hata katika kifo wenye haki hupata kimbilio.
33
Hekima hukaa katika moyo wa mwenye ufahamu bali haijulikani miongoni mwa wapumbavu.
34
Haki huinua taifa, bali dhambi ni aibu kwa watu wote.
35
Mfalme hupendezwa na mtumishi mwenye hekima, bali ghadhabu yake humwangukia mtumishi mwenye kuaibisha.
Settings