Skip to content
Mithali 10:15-21

Mithali 10:15-21

15
Mali ya tajiri ni mji wake wenye ngome, bali ufukara ni maangamizi ya maskini.
16
Ujira wa wenye haki huwaletea uzima, lakini mapato ya waovu huwaletea adhabu.
17
Anayekubali kuadibishwa yuko katika njia ya uzima, lakini yeyote anayepuuza maonyo hupotosha wengine.
18
Yeye afichaye chuki yake ana midomo ya uongo, na yeyote anayeeneza uchonganishi ni mpumbavu.
19
Wakati maneno ni mengi, dhambi haikosekani, lakini yeye ambaye huzuia ulimi wake ni mwenye busara.
20
Ulimi wa mwenye haki ni fedha iliyo bora, bali moyo wa mwovu una thamani ndogo.
21
Midomo ya mwenye haki hulisha wengi, lakini wapumbavu hufa kwa kukosa ufahamu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options