Mithali 10:8-14
8
Mwenye hekima moyoni hupokea maagizo, lakini mpumbavu apayukaye huangamia.
9
Mtu mwadilifu hutembea salama, lakini mtu aendaye katika njia zilizopotoka atagunduliwa.
10
Yeye akonyezaye kwa nia mbaya husababisha huzuni, naye mpumbavu apayukaye huangamia.
11
Kinywa cha mwenye haki ni chemchemi ya uzima, lakini jeuri hufunika kinywa cha mwovu.
12
Chuki huchochea faraka, lakini upendo husitiri mabaya yote.
13
Hekima hupatikana katika midomo ya wenye kupambanua, lakini fimbo ni kwa ajili ya mgongo wake asiye na ufahamu.
14
Wenye hekima huhifadhi maarifa, bali kinywa cha mpumbavu hualika maangamizi.
Settings