Rukia maudhui
Mathayo 8:1-4

Yesu Ashuka na Amtakasa Mwenye Ukoma

Mathayo 8:1-4
1
Yesu aliposhuka kutoka mlimani, makutano makubwa ya watu yakamfuata.
2
Mtu mmoja mwenye ukoma akaja na kupiga magoti mbele yake, akasema, “Bwana, kama ukitaka, unaweza kunitakasa.”
3
Yesu akanyoosha mkono wake akamgusa yule mtu, akamwambia, “Nataka. Takasika!” Mara yule mtu akatakasika ukoma wake.
4
Kisha Yesu akamwambia, “Hakikisha humwambii mtu yeyote. Lakini nenda ukajionyeshe kwa kuhani, na utoe sadaka aliyoamuru Mose, ili kuwa ushuhuda kwao.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options