Rukia maudhui
Mathayo 27:57-61

Kuzikwa kwa Yesu

Mathayo 27:57-61
57
Ilipofika jioni, alifika mtu mmoja tajiri kutoka Arimathaya aitwaye Yosefu, ambaye pia alikuwa mwanafunzi wa Yesu.
58
Akamwendea Pilato ili kumwomba mwili wa Yesu. Pilato akaamuru apewe.
59
Yosefu akauchukua mwili wa Yesu, akaufunga katika kitambaa cha kitani safi,
60
na kuuweka katika kaburi lake mwenyewe jipya, alilokuwa amelichonga kwenye mwamba. Kisha akavingirisha jiwe kubwa katika ingilio la kaburi, akaenda zake.
61
Maria Magdalene na yule Maria mwingine walikuwepo mahali pale, wakiwa wameketi mkabala na kaburi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options