Rukia maudhui
Mathayo 24:32-35

Somo la Mtini

Mathayo 24:32-35
32
“Basi jifunzeni somo hili kutokana na mtini: Matawi yake yanapoanza kuchipua na kutoa majani, mnatambua kwamba wakati wa kiangazi umekaribia.
33
Vivyo hivyo, myaonapo mambo haya yote, mnatambua kwamba wakati u karibu, hata malangoni.
34
Amin, nawaambia, kizazi hiki hakitapita hadi mambo haya yote yawe yametimia.
35
Mbingu na nchi zitapita, lakini maneno yangu hayatapita kamwe.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options