Rukia maudhui
Mathayo 10:1-4

Yesu Awatuma Mitume Kumi na Wawili

Mathayo 10:1-4
1
Ndipo Yesu akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, naye akawapa mamlaka juu ya pepo wachafu, ili waweze kuwatoa na kuponya kila ugonjwa na maradhi ya kila aina.
2
Haya ndiyo majina ya hao mitume kumi na wawili: wa kwanza, Simoni aitwaye Petro, na Andrea nduguye; Yakobo mwana wa Zebedayo, na Yohana nduguye;
3
Filipo, na Bartholomayo; Tomaso, na Mathayo mtoza ushuru; Yakobo mwana wa Alfayo, na Thadayo;
4
Simoni Mkananayo, na Yuda Iskariote aliyemsaliti Yesu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options