Rukia maudhui
Marko 16:9-13

Yesu Awatokea Wanafunzi Wake

Marko 16:9-13
9
Yesu alipofufuka alfajiri na mapema siku ya kwanza ya juma alimtokea kwanza Maria Magdalene, yule ambaye alikuwa amemtoa pepo wachafu saba.
10
Maria akaenda, naye akawaambia wale waliokuwa wamefuatana na Yesu, waliokuwa wanaomboleza na kulia.
11
Lakini waliposikia kwamba Yesu yu hai na kwamba Maria alikuwa amemwona, hawakusadiki.
12
Baadaye Yesu akawatokea wawili miongoni mwa wanafunzi wake walipokuwa wakienda shambani akiwa katika sura nyingine.
13
Nao wakarudi na kuwaambia wenzao. Lakini hawakuwasadiki wao pia.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options