Rukia maudhui
Marko 14:22-26

Kuanzishwa kwa Chakula cha Bwana

Marko 14:22-26
22
Walipokuwa wanakula, Yesu akachukua mkate, akashukuru, akaumega na kuwapa wanafunzi wake, akisema, “Twaeni mle; huu ndio mwili wangu.”
23
Kisha akakitwaa kikombe, akashukuru, akawapa, nao wote wakanywa kutoka humo.
24
Akawaambia, “Hii ndiyo damu yangu ya agano, imwagikayo kwa ajili ya wengi.
25
Amin, nawaambia, sitakunywa tena katika uzao wa mzabibu, hadi siku ile nitakapounywa mpya katika Ufalme wa Mungu.”
26
Walipokwisha kuimba wimbo, wakatoka wakaenda Mlima wa Mizeituni.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options