Sari la conținut
Maombolezo 3:43-53

Maombolezo 3:43-53

43
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
44
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
45
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
46
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
47
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
48
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
49
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
50
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
51
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
52
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
53
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options