Maombolezo 3:40-47
40
Tuzichunguze njia zetu na kuzijaribu, na tumrudie Bwana Mungu.
41
Tuinue mioyo yetu pamoja na mikono yetu kwa Mungu mbinguni, na tuseme:
42
“Tumetenda dhambi na kuasi nawe hujasamehe.
43
“Umejifunika mwenyewe kwa hasira na kutufuatilia; umetuchinja bila huruma.
44
Unajifunika mwenyewe kwa wingu, ili pasiwe na ombi litakaloweza kupenya.
45
Umetufanya takataka na uchafu miongoni mwa mataifa.
46
“Adui zetu wote wamefumbua vinywa vyao wazi dhidi yetu.
47
Tumeteseka kwa hofu kuu na shida ya ghafula, uharibifu na maangamizi.”
Settings