Maombolezo 3:48-54
48
Vijito vya machozi vinatiririka kutoka machoni mwangu, kwa sababu watu wangu wameangamizwa.
49
Macho yangu yatatiririka machozi bila kukoma, bila kupata nafuu,
50
hadi Bwana atazame chini kutoka mbinguni na kuona.
51
Lile ninaloliona huniletea huzuni nafsini kwa sababu ya wanawake wote wa mji wangu.
52
Wale waliokuwa adui zangu bila sababu wameniwinda kama ndege.
53
Walijaribu kukomesha maisha yangu ndani ya shimo na kunitupia mawe;
54
maji yalifunika juu ya kichwa changu, nami nikafikiri nilikuwa karibu kukatiliwa mbali.
Settings