Skip to content
Maombolezo 3:55-66

Maombolezo 3:55-66

55
Nililiitia jina lako, Ee Bwana, kutoka vina vya shimo.
56
Ulisikia ombi langu: “Usikizibie masikio yako kilio changu nikuombapo msaada.”
57
Ulikuja karibu nilipokuita, nawe ukasema, “Usiogope.”
58
Ee Bwana, ulichukua shauri langu, ukaukomboa uhai wangu.
59
Umeona, Ee Bwana, ubaya niliotendewa. Tetea shauri langu!
60
Umeona kina cha kisasi chao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu.
61
Ee Bwana, umesikia matukano yao, mashauri yao yote mabaya dhidi yangu:
62
kile adui zangu wanachonongʼona na kunungʼunikia dhidi yangu mchana kutwa.
63
Watazame! Wakiwa wameketi au wamesimama, wananidhihaki katika nyimbo zao.
64
Uwalipe kile wanachostahili, Ee Bwana, kwa yale ambayo mikono yao imetenda.
65
Weka pazia juu ya mioyo yao, laana yako na iwe juu yao!
66
Wafuatilie katika hasira na uwaangamize kutoka chini ya mbingu za Bwana.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options