Skip to content
Maombolezo 3:27-39

Maombolezo 3:27-39

27
Ni vyema mtu kuchukua nira bado angali kijana.
28
Na akae peke yake awe kimya, kwa maana Bwana ameiweka juu yake.
29
Na azike uso wake mavumbini bado panawezekana kuwa na matumaini.
30
Na atoe shavu lake kwa yule ampigaye, na ajazwe na aibu.
31
Kwa kuwa watu hawakatiliwi mbali na Bwana milele.
32
Ingawa huleta huzuni, ataonyesha huruma, kwa kuwa upendo wake usiokoma ni mkuu.
33
Kwa maana hapendi kuwaletea mateso au huzuni watoto wa wanadamu.
34
Kuwaponda chini ya nyayo wafungwa wote katika nchi,
35
Kumnyima mtu haki zake mbele za Aliye Juu Sana,
36
kumnyima mtu haki: Je, Bwana asione mambo kama haya?
37
Nani awezaye kusema nalo likatendeka kama Bwana hajaamuru?
38
Je, si ni kwenye kinywa cha Aliye Juu Sana ndiko yatokako maafa na mambo mema?
39
Mwanadamu yeyote aliye hai aweza kulalamika wakati anapoadhibiwa kwa ajili ya dhambi zake?
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options