Yohana 1:1-9
1
Hapo mwanzo alikuwako Neno, huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu, naye Neno alikuwa Mungu.
2
Tangu mwanzo huyo Neno alikuwa pamoja na Mungu.
3
Vitu vyote viliumbwa kwa yeye, wala pasipo yeye hakuna chochote kilichoumbwa ambacho kimeumbwa.
4
Ndani yake ndimo ulimokuwa uzima na huo uzima ulikuwa nuru ya watu.
5
Nuru hungʼaa gizani nalo giza halikuishinda.
6
Alikuja mtu mmoja aliyetumwa kutoka kwa Mungu, jina lake Yohana.
7
Alikuja kama shahidi apate kuishuhudia hiyo nuru, ili kwa kupitia kwake watu wote waweze kuamini.
8
Yeye mwenyewe hakuwa ile nuru, bali alikuja kuishuhudia hiyo nuru.
9
Kwamba nuru halisi, imwangaziayo kila mtu ilikuwa inakuja ulimwenguni.
Settings