Ayubu 5:8
Inaonyesha mstari 8 pamoja na muktadha unaouzunguka.
5
Wenye njaa huyala mavuno yake, wakiyatoa hata katikati ya miiba, nao wenye kiu huitamani sana mali yake.
6
Kwa maana taabu haioti kutoka kwenye udongo, wala udhia hauchipui kutoka ardhini.
7
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
Settings