Skip to content
Ayubu 5:8-16

Ayubu 5:8-16

8
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
14
Giza huwapata wakati wa mchana; wakati wa adhuhuri hupapasa kama vile usiku.
15
Humwokoa mhitaji kutokana na upanga ulioko kinywani mwao; huwaokoa kutokana na makucha ya wenye nguvu.
16
Kwa hiyo maskini analo tarajio, nao udhalimu hufumba kinywa chake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options