Ayubu 5:10
Inaonyesha mstari 10 pamoja na muktadha unaouzunguka.
7
Lakini mwanadamu huzaliwa ili kutaabika, kwa hakika kama cheche za moto zirukavyo kuelekea juu.
8
“Lakini ingekuwa ni mimi, ningemlalamikia Mungu, ningeliweka shauri langu mbele zake.
9
Yeye hutenda maajabu yasiyoweza kutambuliwa, miujiza isiyoweza kuhesabika.
10
Yeye huipa nchi mvua, huyapeleka maji kunyesha mashamba.
11
Huwainua juu wanyonge, nao wale waombolezao huinuliwa wakawa salama.
12
Huipinga mipango ya wenye hila, ili mikono yao isifikie ufanisi.
13
Yeye huwanasa wenye hekima katika hila yao, nayo mipango ya wadanganyifu huifagilia mbali.
Settings