Ayubu 40:1-14
1
Bwana akamwambia Ayubu:
2
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
Settings