Ayubu 39:26-30
26
“Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
27
Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
28
Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
29
Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
30
Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”
Settings