Ayubu 39:19-25
19
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
24
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
Settings