Skip to content
Ayubu 39:9-25

Ayubu 39:9-25

9
“Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
10
Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
11
Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
12
Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
13
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
19
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
24
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options