Rukia maudhui
Ayubu 39:13-18

Mbuni asiye na hekima

Ayubu 39:13-18
13
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options