Ayubu 38:22-35
22
“Je, umeshawahi kuingia katika ghala za theluji, au kuona ghala za mvua ya mawe,
23
ambazo nimeziweka akiba kwa ajili ya wakati wa taabu, na kwa ajili ya wakati wa vita na mapigano?
24
Ni ipi njia iendayo mahali umeme wa radi unapotawanyiwa, au mahali upepo wa mashariki unaposambaziwa juu ya dunia?
25
Ni nani aliyepasua mifereji kwa ajili ya maji mengi ya mvua yaendayo kasi na njia ya umeme wa radi,
26
ili kusababisha mvua kunyeshea mahali pasipokaliwa na mtu, jangwa lisilo na yeyote ndani yake,
27
ili kuitosheleza nchi ya ukiwa na jangwa, na majani yaanze kumea ndani yake?
28
Je, mvua ina baba? Ni nani baba azaaye matone ya umande?
29
Barafu inatoka tumbo la nani? Ni nani azaaye ukungu kutoka mbinguni,
30
wakati maji yawapo magumu kama jiwe, wakati uso wa vilindi vya maji unapoganda?
31
“Je, waweza kuufunga mnyororo wa Kilimia? Waweza kulegeza kamba za Orioni?
32
Waweza kuyaongoza makundi ya nyota kwa majira yake, au kuongoza Dubu na watoto wake?
33
Je, unajua sheria zinazotawala mbingu? Waweza kuweka utawala wa Mungu duniani?
34
“Waweza kuiinua sauti yako mpaka mawinguni, na kujifunika mwenyewe na gharika ya maji?
35
Je, wewe hutuma umeme wa radi kwenye njia zake? Je, hutoa taarifa kwako kukuambia, ‘Sisi tuko hapa’?
Settings