Skip to content
Ayubu 38:16-21

Ayubu 38:16-21

16
“Je, umepata kufika kwenye chemchemi za bahari? Au kutembea mahali pa ndani pa vilindi?
17
Umewahi kuonyeshwa malango ya mauti? Umewahi kuiona milango ya uvuli wa mauti?
18
Je, wewe unafahamu ukubwa wa dunia? Niambie kama unajua haya yote.
19
“Njia ya kufika kwenye makao ya nuru ni ipi? Nako maskani mwa giza ni wapi?
20
Je, unaweza kuvirudisha kwenye makao yake? Unajua njia za kufika maskani mwake?
21
Hakika unajua, kwa kuwa ulikuwa umeshazaliwa! Kwani umeishi miaka mingi!
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options