Ayubu 23:8-10
8
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.