Skip to content
Ayubu 23:1-7

Ayubu 23:1-7

1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Hata leo malalamiko yangu ni chungu; mkono wake ni mzito juu yangu hata nikiugua.
3
Laiti ningefahamu mahali pa kumwona; laiti ningeweza kwenda mahali akaapo!
4
Ningeliweka shauri langu mbele zake, na kukijaza kinywa changu na hoja.
5
Ningejua kwamba angenijibu nini, na kuelewa lile ambalo angelisema.
6
Je, angenipinga kwa nguvu nyingi? La, asingenigandamiza.
7
Hapo mtu mwadilifu angeweka shauri lake mbele zake, nami ningeokolewa milele na mhukumu wangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options