Ayubu 23:8-12
8
“Lakini nikienda mashariki, hayupo; nikienda magharibi, simpati.
9
Anapokuwa kazini pande za kaskazini, simwoni; akigeukia kusini, nako simwoni hata kidogo.
10
Lakini anaijua njia niiendeayo; akiisha kunijaribu, nitatoka kama dhahabu.
11
Nyayo zangu zimefuata hatua zake kwa karibu; nimeishika njia yake bila kukengeuka.
12
Sijaziacha amri zilizotoka midomoni mwake; nimeyathamini maneno ya kinywa chake kuliko chakula changu cha kila siku.
Settings