Ayubu 23:13-17
13
“Lakini yeye husimama peke yake; ni nani awezaye kumpinga? Yeye hufanya lolote atakalo.
14
Hutimiliza maagizo yake dhidi yangu, na bado anayo mipango mingi kama hiyo ambayo ameiweka akiba.
15
Hiyo ndiyo sababu ninaingiwa na hofu mbele zake; nifikiriapo haya yote ninamwogopa.
16
Mungu ameufanya moyo wangu kuzimia; yeye Mwenyezi amenitia hofu.
17
Hata hivyo sijanyamazishwa na giza, wala kwa giza nene linalofunika uso wangu.
Settings