Skip to content
Ayubu 21:27-34

Ayubu 21:27-34

27
“Ninayajua kikamilifu yale mnayoyafikiri, mipango ambayo kwayo mngenitendea mabaya.
28
Mwasema, ‘Iko wapi sasa nyumba ya huyo mtu mkuu, mahema ambayo watu waovu walikaa?’
29
Je, hamkuwahi kuwauliza hao wanaosafiri? Je, hamkutafakari taarifa zao:
30
kwamba mtu mwovu huepushwa kutoka siku ya maafa, kwamba huokolewa kutoka siku ya ghadhabu?
31
Ni nani hulaumu matendo yake mbele ya uso wake? Ni nani ampatilizaye kwa yale aliyoyatenda?
32
Hupelekwa kaburini, nao ulinzi ukawekwa kwenye kaburi lake.
33
Udongo ulio bondeni ni mtamu kwake; watu wote watamfuata, nao umati wa watu usiohesabika umemtangulia.
34
“Hivyo ninyi mnawezaje kunifariji kwa upuzi wenu? Hakuna kilichosalia cha majibu yenu isipokuwa uongo!”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options