Skip to content
Ayubu 19:1-9

Ayubu 19:1-9

1
Ndipo Ayubu akajibu:
2
“Je, mtaendelea kunitesa mpaka lini, na kuniponda kwa maneno yenu?
3
Mara kumi hizi mmenishutumu; bila aibu mnanishambulia.
4
Kama ni kweli nimepotoka, kosa langu ninabaki kuhusika nalo mwenyewe.
5
Kama kweli mngejitukuza wenyewe juu yangu, na kutumia unyonge wangu dhidi yangu,
6
basi jueni kuwa Mungu amenitendea yaliyo mabaya, naye amekokota wavu wake kunizunguka.
7
“Ingawa ninalia, ‘Nimetendewa mabaya!’ sipati jibu; ingawa ninaomba msaada, hakuna haki.
8
Yeye ameizuia njia yangu hivyo siwezi kupita; ameyafunika mapito yangu na giza.
9
Amenivua heshima yangu, na kuniondolea taji kichwani pangu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options