Skip to content
Ayubu 14:7-12

Ayubu 14:7-12

7
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options