Skip to content
Mwanzo 11:10-26

Mwanzo 11:10-26

10
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options