Skip to content
Wagalatia 2:1-5

Wagalatia 2:1-5

1
Kisha, baada ya miaka kumi na minne, nilipanda tena kwenda Yerusalemu pamoja na Barnaba, nikamchukua na Tito ili awe pamoja nami.
2
Nilikwenda kwa sababu nilikuwa nimefunuliwa na Mungu, ili nikawaeleze kwa faragha wale walioonekana kuwa viongozi, ile Injili ninayoihubiri kwa watu wa Mataifa. Nilifanya hivyo kwa kuhofia kwamba nisije nikawa nilikuwa ninakimbia au nilikimbia bure.
3
Lakini hata Tito ambaye alikuwa Myunani, hakulazimika kutahiriwa.
4
Lakini kwa sababu ya ndugu wa uongo ambao walijiingiza kwa siri katikati yetu ili kupeleleza uhuru wetu tulio nao katika Kristo Yesu, wapate kututia utumwani,
5
hatukukubaliana nao hata dakika moja, ili kwamba ukweli wa Injili ubaki nanyi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options