Skip to content
Waefeso 6:4

Waefeso 6:4

Inaonyesha mstari 4 pamoja na muktadha unaouzunguka.
1
Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema.
2
“Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi,
3
“upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
4
Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.
5
Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo.
6
Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo.
7
Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options