Waefeso 6:1-9
1
Enyi watoto, watiini wazazi wenu katika Bwana, kwa kuwa hili ni jema.
2
“Waheshimu baba yako na mama yako,” hii ndio amri ya kwanza yenye ahadi,
3
“upate baraka na uishi siku nyingi duniani.”
4
Ninyi akina baba, msiwachokoze watoto wenu, bali waleeni kwa nidhamu na mafundisho ya Bwana.
5
Ninyi watumwa, watiini hao walio mabwana zenu hapa duniani kwa heshima na kwa kutetemeka na kwa moyo mmoja, kama vile mnavyomtii Kristo.
6
Watiini, si tu wakati wakiwaona ili mpate upendeleo wao, bali mtumike kama watumwa wa Kristo, mkifanya mapenzi ya Mungu kwa moyo.
7
Tumikeni kwa moyo wote, kama vile mnamtumikia Bwana na si wanadamu.
8
Mkijua kwamba Bwana atampa kila mtu thawabu kwa lolote jema alilotenda, kama yeye ni mtumwa au ni mtu huru.
9
Nanyi mabwana, watendeeni watumwa wenu kwa jinsi iyo hiyo. Msiwatishe, kwa kuwa mnajua ya kwamba yeye aliye Bwana wenu na Bwana wao yuko mbinguni, naye hana upendeleo.
Settings