Rukia maudhui
Matendo 4:32-35

Waamini washiriki mali zao

Matendo 4:32-35
32
Wale walioamini wote walikuwa na moyo mmoja na nia moja. Wala hakuna hata mmoja aliyesema chochote alichokuwa nacho ni mali yake mwenyewe, lakini walishirikiana kila kitu walichokuwa nacho.
33
Mitume wakatoa ushuhuda wa kufufuka kwa Bwana Yesu kwa nguvu nyingi na neema ya Mungu ilikuwa juu yao wote.
34
Wala hapakuwepo mtu yeyote miongoni mwao aliyekuwa mhitaji, kwa sababu mara kwa mara wale waliokuwa na mashamba na nyumba waliviuza, wakaleta thamani ya vitu vilivyouzwa,
35
wakaiweka miguuni pa mitume, kila mtu akagawiwa kadiri ya mahitaji yake.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options