1 Wathesalonike 5:1-6
1
Basi, ndugu, kwa habari ya nyakati na majira hatuna haja ya kuwaandikia,
2
kwa kuwa mnajua vyema kwamba siku ya Bwana itakuja kama mwizi ajapo usiku.
3
Wakati watu wanaposema, “Kuna amani na salama,” maangamizi huwajia ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwanamke mwenye mimba; nao hakika hawatatoroka.
4
Bali ninyi, ndugu, hampo gizani hata siku ile iwakute ghafula kama mwizi.
5
Ninyi nyote ni wana wa nuru na wana wa mchana. Sisi si wana wa giza wala wa usiku.
6
Kwa hiyo basi, tusilale kama watu wengine walalavyo, bali tukeshe na kuwa na kiasi.
Settings