Rukia maudhui
1 Wakorintho 3:5-9

Watumishi ni Wafanya Kazi Pamoja na Mungu

1 Wakorintho 3:5-9
5
Kwani, Apolo ni nani? Naye Paulo ni nani? Ni watumishi tu ambao kupitia wao mliamini, kama vile Bwana alivyompa kila mtu huduma yake.
6
Mimi nilipanda mbegu, Apolo akatia maji, lakini Mungu ndiye aliikuza.
7
Hivyo mwenye kupanda na mwenye kutia maji si kitu, bali Mungu peke yake ambaye huifanya ikue.
8
Apandaye mbegu ana lengo sawa na yule atiaye maji na kila mmoja atalipwa kulingana na kazi yake.
9
Kwa kuwa sisi tu watendakazi pamoja na Mungu. Ninyi ni shamba la Mungu, jengo la Mungu.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options