Rukia maudhui
1 Wakorintho 16:19-24

Salamu na Baraka ya Kuhitimisha

1 Wakorintho 16:19-24
19
Makanisa ya Asia yanawasalimu. Akila na Prisila, pamoja na kanisa lililoko nyumbani kwao wanawasalimu sana katika Bwana.
20
Ndugu wote walioko hapa wanawasalimu. Salimianeni kwa busu takatifu.
21
Mimi, Paulo, naandika salamu hizi kwa mkono wangu mwenyewe.
22
Kama mtu yeyote hampendi Bwana Yesu Kristo, na alaaniwe. Bwana wetu, njoo.
23
Neema ya Bwana Yesu iwe nanyi.
24
Upendo wangu uwe nanyi nyote katika Kristo Yesu. Amen.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Reading Width 45 chars

Options