Skip to content
1 Nyakati 2:3-15

1 Nyakati 2:3-15

3
Wana wa Yuda walikuwa: Eri, Onani na Shela. Hawa watatu walizaliwa kwake na mkewe Mkanaani, binti wa Shua. Eri, mzaliwa wa kwanza wa Yuda, alikuwa mwovu machoni pa Bwana, kwa hiyo Bwana alimuua.
4
Tamari, mkwewe Yuda, alimzalia wana wawili: Peresi na Zera. Yuda alikuwa na jumla ya wana watano.
5
Wana wa Peresi walikuwa: Hesroni na Hamuli.
6
Wana wa Zera walikuwa: Zimri, Ethani, Hemani, Kalkoli na Dara. Jumla ya wana wa Zera walikuwa watano.
7
Mwana wa Karmi alikuwa: Akari, ambaye alileta taabu kwa Waisraeli kwa kukiuka onyo la kutokuchukua vitu vilivyokuwa vimewekwa wakfu.
8
Mwana wa Ethani alikuwa: Azariya.
9
Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
10
Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
11
Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
12
Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
13
Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
14
wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
15
wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options