1 Nyakati 2:9-17
9
Wana wa Hesroni walikuwa: Yerameeli, Ramu na Kalebu.
10
Ramu alimzaa Aminadabu, na Aminadabu akamzaa Nashoni, kiongozi wa kabila la Yuda.
11
Nashoni akamzaa Salmoni, Salmoni akamzaa Boazi,
12
Boazi akamzaa Obedi, Obedi akamzaa Yese.
13
Yese akawazaa Eliabu mwanawe wa kwanza; wa pili Abinadabu, wa tatu Shimea,
14
wa nne Nethaneli, wa tano Radai,
15
wa sita Osemu, na wa saba Daudi.
16
Dada zao walikuwa Seruya na Abigaili. Wana wa Seruya walikuwa watatu: Abishai, Yoabu na Asaheli.
17
Abigaili alikuwa mama yake Amasa, ambaye baba yake alikuwa Yetheri, Mwishmaeli.
Settings