Skip to content
1 Nyakati 16:8-22

1 Nyakati 16:8-22

8
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake; wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
9
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa; waambieni matendo yake yote ya ajabu.
10
Lishangilieni jina lake takatifu; mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
11
Mtafuteni Bwana na nguvu zake; utafuteni uso wake siku zote.
12
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
13
enyi wazao wa Israeli mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
14
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu; hukumu zake zimo duniani pote.
15
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
16
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
17
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
18
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
19
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
20
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
21
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
22
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
Settings

Reading Style

Typeface

Font Size 19px

Options